Leaders Club kwaendelea kuwaka moto wa burudani
Siku ya tarehe moja mwezi huu wa kumi yaani siku ya jana juma mosi, mambo yalikuwa kabambe pale Leaders Club kwa wasanii, wanamitindo, nyama choma, na kila aina ya starehe zikiwa pale kusherekea miaka 50 ya Uhuru na Bia ya Kilimanjaro ikiungana na Bongo5 Media yenye kumiliki Website ya Bongo5.
Sherehe ilikuwa ya kijamii zaidi, lakini burudani ilikuwa kubwa zaidi, si pa kujilaumu sana kwani siku ya leo tarehe mbili juma pili hii, bado bonanza hilo linaendelea, kwa kiingilio cha shilingi elfu saba, kama jana ulikata ya shilingi elfu kumi basi utaruhusiwa kuendelea kujipatia burudani hiyo.
Baadhi ya michezi iliwemo mchezo wa Kikapu kutoka kwa Lite, yaani mambo yalikuwa juu ya mambo
Wasanii walikuwa wengi waliofanya show kwa siku ya jana, lakini leo pia wapo wengi kwakuwa tamasha ni la masaa 48, hapa alikuwepo Ben Poul
Zaidi ya michezo hiyo, pia kulikuwa na mashindano ya mpira, na kuangalia mpira wa nje kwenye Dstv
wasanii mahili toka Tht, nao walifanya mambo makubwa sana
Kama hujawahi hata kuchezo Golf hata siku moja, basi unaweza kuja na kujifunza… bado haujachelewa
Voice of Afrika, Linex naye alifanya kazi yake vizuri sana
Wakina dada walipendeza kuhakikisha wanakupa huduma iliyonzuri na bora
Hawa nao walikuwepo,