Mchezaji wa mpira wa kikapu nchini Marekani, LeBron James ameamua kujiunga na shule ambayo amewahi kusoma huko Ohio huku akiwa na kibarua cha kuitumikia Los Angeles Lakers kwenye msimu wake wa kwanza.
James mwenye umri wa maiaka 33 kupitia mtandao wake wa kijamii posti picha zinazomuonyesha akifanya mazoezi kwenye ‘gym’ ya shule ya St. Vincent–St. Mary High School ambayo amejiunga.
LeBron James ambaye amejiunga na Los Angeles Lakers akitokea Cleveland Cavaliers aliyoanza kuitumikia tangu mwaka 2014 ameeleza kuwa anachohitaji yeye ni kuifanya shule hiyo aliyopata kusoma hapo hawali kujivunia uwepo wake baada ya kuwa mchezaji mwenyethamani kubwa.
”Hakuna ninachopenda kama kuwa sehemu ambayo sote tunaanzia maisha ya kazi,” ameandika James akiwa ndani ya shule hiyo.
LeBron James ameongeza ”’Najihisi ni mwenyefaraja kubwa. Napenda kile St. Vincent–St. Mary High School kilichonifanyia wakati nilipokuwa nikija shule na kuondoka.”
James mara kadhaa amekuwa akirudisha fadhila kwa jamii na hata kuchangia dola milioni moja kwenye shule hiyo.