Michezo
Leeds United yamtimua kocha wake, Paul Heckingbottom
Klabu ya Leeds United ya nchini Uingereza imeachana na kocha wake, Paul Heckingbottom baada ya kuiyongoza timu hiyo kwa muda wa miezi minne pekee.
Ripoti zanaeleza kuwa aliyekuwa kocha wa Argentina, Athletic Bilbao na Marseille, Marcelo Bielsa huwenda akawa mrithi wa Heckingbottom.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 40, aliachana na klabu yake ya zamani ya Barnsley mwezi Februari na kujiunga na Leeds iliyomaliza nafasi ya 13 kwenye ligi ya Sky Bet Championship.