Habari
Legend wa muziki wa Reggae Alpha Blondy kutumbuiza Kenya leo
Je wewe ni mpenzi wa Reggae? Na je wewe ni shabiki wa kweli wa Alpha Blondy? Well habari njema ni kuwa Alpha Blondy hivi sasa unavyosoma habari hii hayuko mbali ‘sana’ na wewe kama upo Tanzania, ila habari mbaya kwako ni kuwa hayuko karibu ‘sana’ na wewe sababu yupo nchi jirani ya Kenya na anategemewa kutumbuiza leo
Alpha Blondy alipokuwa akiwasili Kenya jana
Reggae Icon huyo kutoka Ivory Coast ametua nchini Kenya jana Ijumaa (June14) tayari kwa kutumbuiza katika tamasha la Big Tunes linalofanyika leo Jumamosi (June 15) jijini Nairobi.
Alpha Blondy atapanda jukwaa moja na msanii mwingine kutoka Jamaica aitwaye Tarrus Riley.
Picha: Daily Post