Michezo

Leicester City yavinyong’onyeza vigogo vya EPL vinavyomtaka Vardy

Timu inayoshika usukani wa kuongoza ligi kuu ya Uingereza, Leicester City imetangaza kuwa thamani ya Vardy ni paundi milioni 30 kwa timu ambazo zinazomtaka kumsajili mchezaji huyo.

02_08075105_6e5bfc_2729405a

Leicester City ambayo inaongoza ligi kuu ya Uingereza ikiwa na pointi 60, huku wakipewa nafasi kubwa ya kuchukuwa kombe hilo la ligi kuu nchini humo. Vigogo wa ligi hiyo tayari wameshakata tamaa ya kuwania kombe hilo.

Mpaka sasa Vardy, 29 ameshaifungia timu yake ya Leicester magoli 19 kwenye mashindano yote ambayo timu hiyo imeshiriki msimu huu. Mkataba wa Vardy unaisha 2019 baada ya hivi karibuni kusaini mkataba wa miaka mitatu ambao unamfanya alipwe paundi 80,000 kwa wiki.

01_08075105_f97cb3_2729407a

Timu za Chealsea, Manchester United na wengine wanaonekana kumnyatia mchezaji huyo kutokana na kuvutiwa na ufungaji wake bora wa magoli na uchezaji wake mzuri wa kujiamini akiwa uwanjani.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents