Michezo
Ligi kuu ya England kuendelea Jumanne hii
Ligi kuu ya England itaendelea tena jumanne baada kuwa katika mapumziko kufuatia michuano ya FA, kwa michezo mbali mbali, Arsenal watawakaribisha Southampton,Leicester city watakuwa wenyeji wa Liverpool, Norwich watakuwa wakimenyana na Tottenham Hotspurs.
Michezo mingine Sunderland watawaalika Manchester City, Aston Villa watakuwa wageni wa West Ham United,Crystal Palace watawakaribisha Bournemouth, Stoke watakuwa wenyeji wa Manchester Unted na West Brom watachuana na Swansea city.
Hadi sasa Leicester city wanaongoza ligi kwa alama 47 ikifuatiwa na Manchester city katika nafasi ya pili,nafasi ya tatu ni Arsenal na nafasi ya nne ni Tottenham.