Burudani
Lil Wayne aruhusiwa kutoka hospitali
Afya ya Lil Wayne imeanza kuimarika.
Jumapili iliyopita rapper huyo alipigwa na kifafa akiwa hotelini na kukimbizwa hospitali akiwa hajitabui. Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, umeripoti kuwa Wayne ameruhusiwa kutoka hospitalini alipokuwa amelazwa mjini Las Vegas.
Kwa ujibu wa taarifa iliyotolewa na madaktari, rapper huyo amedaiwa kutakiwa kupumzika kwa kipindi cha wiki mbili bila ya kufanya kazi yoyote ikiwemo kupanda jukwaani kutumbuiza.
Kwa hiyo Lil Wayne atatarajiwa kuonekana tena jukwaani kwenye tamasha lake la mwezi Septemba 23 ya mwaka huu.