Michezo

Lionel Messi kutua Italia kumkabili Ronaldo ligi ya Serie A 

Lionel Messi kutua Italia kumkabili Ronaldo ligi ya Serie A 

Vita ya wachezaji pendwa zaidi duniani katika soka, Cristiano Ronaldo na Lionel Messi haijafika mwisho baada ya wawili hao kuwa kwenye ligi tofauti.

Mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi

Ronaldo aliyetoka Madrid na kusajiliwa na Juventus ya Italia baada ya utawala wake wa misimu tisa Laliga ameonekana kama ametengana na mpizani wake Messi aliyebaki nchini Hispania lakini kwa sasa mambo huwenda yakabadilika kwa wawili hao kukutana tena kwenye ligi moja ambayo ni Serie A ya nchini Italia.

The Portuguese star left Madrid for Turin in an £88million move this summer for a 'challenge'

Mshambuliaji wa Juventus, Cristiano Ronaldo

Kwa mujibu wa taarifa kutoka nchini Italia klabu ya Inter Milan inahusishwa kutaka kumsajili mshambuliaji hatari wa Barcelona, Lionel Messi ili kuleta ushindani kwenye ligi ya Serie A dhidi ya Juventus ambao wamekamilisha dili la kuingia kandarasi na Cristiano Ronaldo.

Front page of Tuttosport focuses on Inter wanting 'Messi to rival Cristiano Ronaldo at Juventus'

Wadhamini wa kuu wa klabu ya Inter Milan ambao ni kampuni ya Pirelli kupitia Mkurugenzi mtendaji wake, Marco Tronchetti Provera katika mahojiano yake amesema kuwa mmiliki wa timu hiyo ambayo ni Suning ikiwa chini ya Zhang Jindong inatarajia kufanya usajili mkubwa mno kabla ya dirisha la usajili kufungwa.

Inter fan and Pirelli CEO Marco Tronchetti Provera suggested nobody could 'say no to Messi'

Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Pirelli, Marco Tronchetti Provera

Tronchetti Provera katika mahojiano yake amekwenda mbali zaidi na kusema kuwa anaimani Suning inaweza kufanya usajili mkubwa sana na kuhoji kwa nini isiwezekane kuwa ni Messi.

Messi mwenye umri wa miaka 31, ameingia mkataba wa muda mrefu na klabu ya Barcelona unaomuweka hapo mpaka msimu wa mwaka 2021.

Related Articles

13 Comments

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents