Lionel Messi kutua Italia kumkabili Ronaldo ligi ya Serie A
Lionel Messi kutua Italia kumkabili Ronaldo ligi ya Serie A
Vita ya wachezaji pendwa zaidi duniani katika soka, Cristiano Ronaldo na Lionel Messi haijafika mwisho baada ya wawili hao kuwa kwenye ligi tofauti.
Mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi
Ronaldo aliyetoka Madrid na kusajiliwa na Juventus ya Italia baada ya utawala wake wa misimu tisa Laliga ameonekana kama ametengana na mpizani wake Messi aliyebaki nchini Hispania lakini kwa sasa mambo huwenda yakabadilika kwa wawili hao kukutana tena kwenye ligi moja ambayo ni Serie A ya nchini Italia.
Mshambuliaji wa Juventus, Cristiano Ronaldo
Kwa mujibu wa taarifa kutoka nchini Italia klabu ya Inter Milan inahusishwa kutaka kumsajili mshambuliaji hatari wa Barcelona, Lionel Messi ili kuleta ushindani kwenye ligi ya Serie A dhidi ya Juventus ambao wamekamilisha dili la kuingia kandarasi na Cristiano Ronaldo.
Wadhamini wa kuu wa klabu ya Inter Milan ambao ni kampuni ya Pirelli kupitia Mkurugenzi mtendaji wake, Marco Tronchetti Provera katika mahojiano yake amesema kuwa mmiliki wa timu hiyo ambayo ni Suning ikiwa chini ya Zhang Jindong inatarajia kufanya usajili mkubwa mno kabla ya dirisha la usajili kufungwa.
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Pirelli, Marco Tronchetti Provera
Tronchetti Provera katika mahojiano yake amekwenda mbali zaidi na kusema kuwa anaimani Suning inaweza kufanya usajili mkubwa sana na kuhoji kwa nini isiwezekane kuwa ni Messi.
Messi mwenye umri wa miaka 31, ameingia mkataba wa muda mrefu na klabu ya Barcelona unaomuweka hapo mpaka msimu wa mwaka 2021.
Nimesikia hizi taarifa asubuhi ya leo kuwa AC Milan wanamhitaji kwa udi na uvumba pamoja na manemane huyu mtaalam halisi wa soka na sio kama yule bishoo mwengine!
Itapendeza
Utamuona tu anaetemberea nyota za watu anafwata nn
Kama kweli itabamba kinomanoma serie A
Hivyo vyanzo vya habar mnavitoa wap
Messi ni kafara wa Barcelona hawez kutok mana anajuw akitok na byak binaisha juu ni muchezaji wakusaidiwa sio wakujitegemea
Pombe sio maji kaka hebu tuliza… labda ulidhani ni cr7 ndio unazungumzia…
Akl mgando zngne shda tu kuna mchezaj ambae hapat msaada toka kwa wenzake au bhangi ndio inaongea
Hamna club ya maan Italy yenye hadhi ya kua na MTU km Messi tofaut na juventus ao wte walobak mbarara tu alpoenda Ronaldo ni sahh
Tatizo watu huwa tunawek ushabiki mbele na kupinga ukweli nambie team ya taïfa anasaidiaga nini ila renaldo kuanzia fc porton man utd réal Madrid na Sasa yu juventus nadahani uyo ni ushahidi tosha
Team gan ya kumchukua messi, hizo pesa wanazo za kumsajiri.
Damn… Bt cR7 greaT
Wat a joke ” messi ni mkubwa” WA mafanikio ” kuliko hizo club zote za italia ” hawezi toka Spain aisee