Habari

Lissu ameweza kula vizuri – Lema

Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema amesema kuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu anaendelea vizuri na ameweza kula na kuongea na watu.

Mhe. Lema ametumia ukurasa wake wa Twitter kuelezea hali ya Mbunge huyo ambapo mara kwa mara amekuwa akitumia ukurasa huo kutoa taarifa za afya ya mbunge huyo.

“Mh Lissu anaendelea vyema hospital . Leo ameweza kula vizuri na kuongea na watu wengi zaidi. Asanteni kwa sala zenu. Mungu awabariki sana,” ametweet Lema.

Mbunge Lissu aliyejeruhiwa tarehe 7, Septemba kwa kupigwa risasi eneo la ‘area D’ mjini Dodoma na watu wasiojulikana.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents