Michezo

Liverpool kufanya usajili wa kibabe, Kylian Mbappe ‘In’, Sadio Mane ‘Out’ 

Klabu ya Liverpool imepanga kumsajili nyota wa Paris Saint-Germain superstar Kylian Mbappe kwa kubadilishana na mchezaji wao, Sadio Mane na kitita cha paundi milioni 200.

Liverpool line up swoop for Kylian Mbappe as replacement for £150m ...

Kama usajili huo utafanikiwa utaandika historia nyingine kwenye mchezo wa soka baada ile ya Neymar kutoka Barcelona mwezi Agosti mwaka 2017 na kujiunga na PSG kwa dau nono kama hilo.

Liverpool Target Kylian Mbappe if Sadio Mane Leaves for Real ...

Kwa mujibu wa The Sun inadaiwa Mabosi wa Liverpool wana wasiwasi na mustakabali wa Sadio Mane, ambaye mpaka sasa bado hajakubali kuongeza kandarasi mpya ya kuendelea kusalia Anfield.

Liverpool wamejipanga kuhakikisha wanafanya usajili mkubwa kunako dirisha lijalo la usajili, huku wakiwa hawana uhakika wa kumbakiza nyota wao Mane.

Sadio Mane amekuwa katika wakati mzuri msimu huu, akiwa tayari na jumla ya magoli 14 akichangia pasi za mwisho tisa (9) zilizozalisha magoli kwenye michezo yake 26 ya Premier League

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents