Michezo

Liverpool roho juu baada ya kuumia Mo Salah wakati anaitumikia timu yake ya taifa

Wakati anaitumikia timu yake ya taifa Mafarao

Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Misri pamoja na klabu ya Liverpool Mo Salah amepata majereha siku ya jana ijumaa wakati anaitumikia timu yake ya taifa.

Salah alipata majeruhi hayo huku akiisaidia timu hiyo kupata ushindi mkubwa dhidi ya timu ya Swaziland wa jumla ya goli 4-1,huku Salah akifunga goli linalotajwa kuwa ni goli bora kwa mafarao hao baada ya kupiga kona iliyoingia moja kwa moja golini.

Mshambuliaji huyo wa Liverpool alipata majeruhi dakika ya 88 ya mchezo huo wa kufuzu katika michuano ya AFCON,Goli la jana la Mo Salah lilimfanya afikishe jumla ya magoli 40 katika timu yake ya taifa.

Ingawa majeraha yake hayo ya msuli yanatajwa kuwa sio makubwa sana baada ya kuumia misuli,majeraha ambayo yanaiweka roho juu klabu ya Liverpool kwani ni moja ya wachezaji tegemezi katika klabu hiyo kubwa katika ligi kuu Engalnd.

Licha ya Liverpool kuwa katika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi ikiwa na alama 20 ikiwa na vinara Man City pamoja na Chelsea ingawa zinapishana kwa wingi wa magoli ya kufunga na kufungwa, siku ya jumamosi ya tarehe 20 mwezi huu klabu ya Liverpool itakuwa uwanjani kwa kuwafuata Huddersfield Town katika dimba la John Smith’s linalomilikiwa na klabu ya Huddersfield Town.

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents