Michezo

Liverpool vs Man United kukutana kwenye fainali ya International Champions Cup

Mahasimu katika ligi kuu ya Uingereza, Liverpool na Manchester United wanakutana leo katika fainali ya International Champions Cup mjini Miami.

article-2715016-203C453A00000578-1000_634x457
kikosi cha Van Gaal kikijianda na mechi ya leo dhidi ya Liverpool

Liverpool wameingia katika hatua hiyo ya fainali baada ya kuifunga Ac Milan 2-0 katika hatua ya nusu fainali huku Man United wakiifunga Madrid magoli 3-1 nakuingia fainali.

1407108614456_wps_5_MIAMI_FL_AUGUST_03_THE_SU
Wachezaji wa The Reds ‘wakipasha’ kabla ya mechi ya leo dhidi ya Manchester United

Mara ya mwisho watani hawa wajadi walikutana na Liverpool walishinda magoli 3-0 dhidi ya Man United katika mechi ya mzunguko wa pili wa ligi kuu. Hii ni mara ya kwanza kwa makocha Brendan Rodgers na Van Gaal kukutana kabla ya ligi kuu ya Uingereza kuanza tarehe 16 August.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents