Michezo
USAJILI: Liverpool waitosa Barcelona
Klabu ya Liverpool imekataa kumuachia mshambuliaji wake, Philippe Coutinho kwenda Barcelona kwa dau la Euro milioni 90.
Dili la Euro milioni 90 ni la pili kukataliwa baada ya vijogoo hao wa Anfield, Liverpool kuwachomolea dili la kwanza la Euro milioni 76.
Hata hivyo mbio za Klabu ya Barcelona za kutaka kunasa saini ya Coutinho (25) huenda zikaishia njiani kwani klabu ya Liverpool tayari imeshatangaza kuwa haina mpango wa kumuuza mshambuliaji huyo msimu huu.
SOMA ZAIDI Barcelona yathibitisha kuondoka kwa Neymar
Klabu ya Barcelona inahaha kutafuta mchezaji mbadala wa Neymar Jr ambaye amehama klabuni hapo na kujiunga na matajiri wa Ufaransa, PSG kwa dau la Euro milioni 222 na kuweka rekodi ya mchezaji wa mpira ghali zaidi kununuliwa duniani.