Michezo
Liverpool yamsajili nyota wa Brazil baada ya kuizidi kete Man United
Club ya Liverpool imemsajili rasmi mshambuliaji wa Brazil, Roberto Firmino,23 kutoka klabu ya Hoffenheim kwa dau la paundi milioni 29. Mchezaji huyo awali alikuwa akiwaniwa na Manchester United.
Roberto Firmino anakuwa mchezaji wa pili aghali kusajiliwa katika historia ya Liverpool kwa ada ya paundi milioni 29 na amekubali kusaini mkataba wa miaka mitano wenye thamani ya paundi 100,000 kwa wiki. Kwa sasa anasubiri vipimo vya afya Anfield mara tu baada ya Copa America kumalizika.