Lord Eyez Kufungua Milango ya Nako 2 Nako.
Ni mwanajeshi toka pande za North hakunaga mwingine ni maneneo yake msanii na kiongozi wa kundi la Nako 2 Nako Lord Eyez ambaye anatarajia kujikata na kuelekea nchi kadhaa za ulaya kwa ajili ya kufanya maonesho
Ni mwanajeshi toka pande za North hakunaga mwingine ni maneneo yake msanii na kiongozi wa kundi la Nako 2 Nako Lord Eyez ambaye anatarajia kujikata na kuelekea nchi kadhaa za ulaya kwa ajili ya kufanya maonesho na hili atalifabikisha mara atakapomaliza kukamua kwenye show ya tarehe 28 Leaders Club mwishoni mwa mwezi huu.
Akizungumza na mwandishi wa Bongo5 alisema natarajia kutimba nchi kibao lakini nyingine ni kwa ajili ya matembezi na shughuli zangu za kisanii ila nitapiga show Uingereza, Norway na Netherlands na kuna manchi kibao yanahitaji nikapige show lakini bado hatujaafikiana kimkwanja-Lord Eyez.
Katika safari hiyo anatarajia kuongozana na mamsapu wake ambaye nae ana ziara katika nchi 12 tofauti ikiwepo marekani, huyu si mwingine bali ni Binti Kiuno a.k.a Ray 2 Tha C jina halisi Rehema Ray C Chalamila, mmoja kati ya wasanii wa kibongo wanaopiga sana vimeo katika nchi za watu. katika vitu ambavyo sitaacha kuvifanya mara nitakapotua nitamtafuta mtu mzima ZiggyLah wa kundi la X-Plastaz kwa ajili ya kupiga nae mikono kadhaa kwenda kuifungua milango ya WaNako.
Jamaa hao ambao wanakomaa na kuitangaza albam yao inayokwenda kwa jina la hawahemi streets hustler Vol 1 ambayo inapatikana mitaani hivi sasa.