Habari

Lord Eyez: Naomba tuipe muda mahakama naamini ntapata haki yangu

Rapper wa kundi la Weusi, Lord Eyez amewataka wananchi kuiachia mahakama iamue hatma yake na kujizuia kumuita mhalifu kwakuwa bado chombo hicho cha sheria hakijatoa maamuzi yake.

Rapper huyo ametoa wito huo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa hoteli ya Double View iliyopo Sinza jijini Dar es Salaam.

Lord Eyez alikuwa ameambatana na mwanasheria wake Peter Kibatala pamoja na members wenzie wa Weusi, Nikki wa Pili na G-Nako.

“Naomba tuipe muda mahakama naamini ntapata haki yangu na uhakika Mungu yuko pamoja nami na mafans wangu poleni sana naomba mnipe nafasi yenu nipate haki yangu niendelee kulisha madini sababu ninayo mengi lakini nimekuwa na misukosuko mingi ambayo Mungu pekee ndio anaweza kujua ukweli,” alisema Lord Eyez.

Unajua maisha yana milima na mabonde ndio nimekuwa mtoto wa kiume naweza kuvumilia lakini ni wakati mgumu sana kwangu na vitu ambavyo sijazoea, nimepitia maisha ambayo sijawahi kuyaona mengine,lakini all in all King Eazy kuna trak mpya inakuja so keep tuning, media support nini cause am not a criminal.”

Kwa upande wake mwanasheria wake ambaye alisema lengo la kukutana na waandishi wa habari ni kuweka ‘record’ sawa tofauti na watu walivyolisikia tuki hilo, alidai kuwa tarehe 20 mwezi uliopita Lord Eyez alipigwa simu na mtu ambaye walikuwa wamefahamiana kwa muda mfupi na kuamini kuwa alimtaka kwenda kuzungumza masuala ya kijamii.

Alipofika katika eneo hilo ambapo ametaja kuwa ni Kinondoni, Lord Eyez alikutana na kundi la watu ambapo wawili anawafamu lakini alidai hawezi kuwataja kwasababu za kisheria. Alisema baada ya muda mteja wake alivamiwa na watu kama 15 waliokuwa kwenye magari matatu ambao walisema wanamshuku kuiba vifaa vy gari na kumweka chini ya ulinzi kwa masaa yasiyopungua matatu huku wakimshinikiza akiri kuhusika na wizi wa vifaa hivyo.

Baada ya hapo ndipo alipopelekwa polisi. Mwanasheria huyo alidai kuwa Lord Eyez aliwekwa mahabusu kwa zaidi ya siku 10 kitu ambacho ni kinyume cha sheria kwa mtuhumiwa kukaa bila kupelekwa mahakamani.

Aliongeza kuwa si jambo jema kwa wananchi kuhitimisha kwa kudai kuwa tayari Lord Eyez ni mhalifu na amehusika kwenye tukio hilo kwakuwa bado mahakama haijaamua hivyo.

“Jamii itoe nafasi kwa mchakato huu wa kisheria uweze kutoa majibu, majibu hayo ndio watu wanaweza kuyafanyia kazi,” alisisitiza.

Amesema taarifa hizo zimemwathiri mteja wake hasa kwakuwa anategemea zaidi mapokeo chanya ya mashabiki wake ili kazi zake ziweze kufanikiwa hivyo ana haki ya kuendelea kuitwa mtuhumiwa tu wa jambo hilo.

Amesema yeye na mteja wake wanafikiria kuandaa mchakato wa kisheria ili kuwashughulikia wale waliohusika na kusambaza habari za kumchafua kimakusudi wakati ambapo vyombo vya sheria havijatoa uamuzi sahihi.

Kwa upande wake Lord Eyez amewataka mashabiki wake wake na subira wakati ambapo mahakama inaendelea na mchakato wa kutoa maamuzi yake.

Naye Nikki wa Pili alidai kuwa tukio hilo limewaweka Weusi katika wakati mgumu kwakuwa wamekuwa wakisumbuliwa na watu wengi kutaka walizungumzie suala hilo lakini wamekuwa kimya kwakuwa walitaka lizungumziwe kisheria zaidi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents