Michezo
Louis van Gaal azitaja sababu za kutaka kumtema Victor Valdes
Kocha wa Manchester United, Louis van Gaal anaonekana kumwonyesha mlango wa kutokea Old Trafford mlinda mlango, Victor Valade baada ya kuonekana hana nidhamu.
Louis van Gaal akiongea na waandishi wa habari nchini Marekani
Kocha huyo alibainisha kuwa Valdes alikataa kuichezea timu ya pili msimu uliopita.
Anadai kuwa Valdes ameshindwa kuendana na falsafa zake ndani ya kipindi kifupi klabuni hapo.
Valdes alijiunga Manchester United kwa uhamisho huru Januari baada ya kuondoka Barcelona 2014. Na sasa United wako tayari kumuuza Mhispania huyo aliyeachwa katika kikosi hicho kilichopo ziarani nchini Marekani.