Ludacris atifua msimu wa Dhahabu
KATIKA msimu wa Serengeti Fiesta2011 uliofanyika katika viwanja vya Leader’s Club, ulikuwa wa aina yake baada ya mwanamuziki toka Marekani Ludacris kutua kwenye viwanja hivyo na kushusha bonge la burudani.
Mwanamuziki huyo ambaye alisindikizwa na wasanii wa nyumbani wapatao 45, waliweza kufanya bonge la shoo la kuhitimisha msimu huo wa Dhahabu kwa kanda ya Dar es salaam . Pia kuna wasanii wamejaribu kufanya vizuri, zaidi kuliko walivyotegemewa, akiwepo Daimondo, Roma, Mwana Fa, na wengine wengi.
Clouse Fm pia walitoa tuzo kwa wasanii ambao walikuwepo kwenye Fiesta mbaslimbali na kuonyesha mchango wao, baadhi ya wasanii waliopokea tuzo hizo ni Prof J, Juma Nature, Mr Nice, Mandojo na Domo kaya, Lady Jay Dee, Dully Syskes,
Maandalizi yakiendelea kwaajili ya kupanda Ludacris baada ya ya kumaliza kwa wasanii wa ndani.
Juma Kasim Nature akiimba na kundi la Wachuja nafaka, akiwemo Dolo, Kr, na mmoja wa waimbaji wa Mabaga Fresh
Adam Mchomvu, Fetty na B Dazen Ma Mc katikata tamasha
Mambo yalikuwa full bata kwenda mbele huku bia yako ya Serengeti pembeni
Roma naye alikuwepo kukamilisha show ya Fiesta2011
Wanadada wakitimiza haja yako ya kukuletea kinywaji popote ulipo wakati wa tamasha
Dady!!!! Pindi alipopata Prof J ndilo jina la kwanza kuitwa.
{hwdvideoshare}id=1543|width=400|height=300|tpl=playeronly{/hwdvideoshare}
{hwdvideoshare}id=1542|width=400|height=300|tpl=playeronly{/hwdvideoshare}
{hwdvideoshare}id=1547|width=400|height=300|tpl=playeronly{/hwdvideoshare}
{hwdvideoshare}id=1546|width=400|height=300|tpl=playeronly{/hwdvideoshare}