Michezo

Luis Enrique akubali kupokea kijiti kutoka kwa Antonio Conte

Habari kutoka Hispania zinaeleza kuwa meneja wa zamani wa klabu ya Barcelona, Luis Enrique ameonekana kukubali kurithi mikoba ya kocha Antonio Conte ndani ya Chelsea.

Luis Enrique kurithi mikoba ya Conte ndani ya Chelsea

Nafasi ya Conte ndani ya kikosi cha Blues imeonekana kuwa mashakani tangu wiki iliyopita baada ya kupata matokeo mabaya ya kufungwa 3 – 0 dhidi ya Bournemouth na yale ya 4-1 mbele ya Watford siku ya Jumatatu.

Kufuatia mwenendo wa kusuasua kwa kikosi cha Chelsea mmiliki wa timu hiyo Mromania Abramovich anampango wa kumpatia mkataba wa miaka miwili na nusu kocha Enrique mwenye umri wa miaka 47 ambao atakuwa the blues hadi mwaka 2020 hii ni kwa mujibu wa chombo cha Sports.

Meneja wa zamani wa klabu ya Barcelona, Luis Enrique

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents