Michezo
Lukas Podolski atangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa Ujerumani
Mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Ujerumani na klabu ya Galatasaray Lukas Podolski ametangaza rasmi kustaafu kuichezea timu yake ya taifa.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Bayern Munich,Arsenal ameamua kutundika daruga akiwa ameichezea timu hiyo mechi 129 akifunga magoli 48.
Podolski ,31, ameanza kuichezea timu ya taifa ya Ujerumani mwaka 2004 na alikuwepo katika kikosi cha mwaka 2014 kilichochukua ubingwa wa kombe la dunia nchini Brazil.