Luku yawa tatizo
Baada ya watu wa jijini Dar es salaam kuingia kwenye mgao mkubwa wa umeme lakini kuanzia jumatatu hadi leo wamejikuta wakiingia kwenye zahama lingine la kukosekana kwa vocha za Luku ya umeme baada ya mawasiliano ya mtandao wa luku kugoma kufanya kazi. Wengi wao wamejikuta wakikesha kutwa nzima
kwenye vituo vya luku na hatmaye wanajikuta wakiondoka bila ya hata umeme kwenye vituo hivyo. Baadhi ya vituo vilifunga sehemu zao za biashara mapema kwa maana kwamba huduma hiyo kwa siku hiyo haipatikani, lakini vituo vingine vilikuwa wazi huku wateja wakisubiri kwa tumaini la kupata umeme lakini hatmaye mpaka saa tano usiku hakuna chochote kinachoendelea na kuondoka kama walivyokuja.
Kituo hiki cha ‘Manzese chenyewe kiliandika kwa ‘Hakuna Huduma Leo’ kwa maana huduma haitopatikana kwa siku hiyo.
Wengi wa wateja walishauri kama vocha hizo za luku ziweze kuuzwa kama vocha za simu, kwani kufanya hivyo kutapunguza matatizo yasiyokuwa ya lazima kama ilivyokuwa kwa siku mbili hizi