Bongo Movie
Lulu akiwa Mahakama Kuu kesi ya kuua, Mama Kanumba atia huruma (Video)
Mama Kanumba alikuwa ni mmoja kati ya watu waliohudhuria kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili, Elizabeth Michael ‘Lulu’ Mahakama Kuu jijini Dar es salaam. Mama huyo ambaye kwa sasa na yeye ametupa karata yake kwenye filamu, alionekana kutokuwa na furaha hali ambayo iliibua hisia ya huruma kwa watu waliojitokeza Makamani hapo. Kesi hiyo itaendelea kusikilizwa kesho baada ya shahidi mmoja upande wa Jamhuri, Seth Bosco ambaye ni mdogo wake Kanumba kutoa ushahidi wake mbele ya jaji, Sam Rumanyika.