Burudani
Lulu Diva kuwaonesha ‘Utamu’ mashabiki wake leo usiku
Baada ya kuachia ‘Usimwache’, Lulu Diva leo usiku anatarajia kuwaonesha mashabiki wake kichupa cha wimbo wake mpya ‘Utamu’ ambao umekuwa gumzo kwa sasa hapa nchini.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram amethibitisha taarifa hizo kwa kuandika “Leo Usiku UTAMU VIDEO Inatambulishwa kwenye tambala lako la EATV ndani ya Friday Night Live na @sammisago Usikoseeeee!! Directed By @Hanscana.”
Lulu Diva ambaye ngoma yake ya Usimwache bado inafanya vizuri kwenye Media ni moja ya wasanii ambao kwa mwaka huu mpaka sasa wamemaintain kwenye game kwa kutoa ngoma kali .