Burudani
Luteni Kalama adai ndoa haiwezi kuathiri muziki wake
Rapper wa kundi la Gangwe Mob, Luteni Kalama, amewahakikishia mashabiki wake kuwa hatua ya kufunga ndoa hivi karibuni, haitaathiri muziki wake.
Hivi karibuni Luteni Kalama alimvisha pete ya uchumba mpenzi wake wa siku nyingi, Bella aliyewahi kuwa Miss Ruvuma.
Luteni amesema kuwa kama kipaji cha mtu kipo hakiwezi kupotea.
“Ukijiamini kama jina la Luteni Kalama litabaki siku zote katika sanaa,” aliiambia E-News ya EATV.
Kwa upande mwingine, Kalama alisema kuna ujio mpya wa kundi la Gangwe Mob. “Kuna rekodi kama tatu ambazo zitatoka kati ya sasa na mwezi wa 7,” alisema.