Burudani
M2 The P anatarajia kupata mtoto, adai ataitwa Mangwea
Msanii wa muziki, M2 The P anatarajia kupata mtoto ambapo amedai kama akizaliwa mtoto wa kiume basi atampatia jina Mangwea ili kuendelea kumuenzi rafiki yake Albert Mangwea aliyefariki dunia miaka kadhaa iliyopita.
M2The P na mpenzi wake
Akizungumza na Bongo5 Jumapili hii, M2The 2 amedai mpenzi aliyenaye kwa ni mjamzito.
“Tunamshukuru Mungu mpenzi wangu ni mama kijacho,” alisema M2The P huku akitabasamu kwa huraha. “Mambo yakienda sawa na akajifunga mtoto wa kiume basi mtoto wangu ataitwa Mangwea, nadhani sina chakueleza sana jinsi nilivyo kuwa mimi na Albert Mangwea,”
Pia rapa huyo amewataka mashabiki wa muziki kusubiria video yake mpya aliyoshoot Afrika Kusini.