Siasa

Maalim Seif: Membe alishiriki vikao vya ndani kumuunga mkono Lissu (+Video)

Mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo anayewania tiketi ya urais Zanzibar Seif Sharif Hamad amesema amesikitishwa sana na majibu ya Bernad Membe kuwa ataendelea na kampeni za kuwania nafasi ya urais.

Maalim Seif amesema hilo limemshangaza sana kwani wakati tangu anajiunga cha ACT Wazalenzo walimwambia nia yao ya kushirikiana na vyama vingine.

Maalim amesema kampeni zao zilikuwa zinasuasua hata kupata wadhamini hivyo wakakaa kikao wakati Membe akiwepo na kushauriana kuwa mgombea wetu haonekani, hivyo tumuunge mkono Lissu.

‘’Kamati ya uongozi pamoja na Membe mwenyewe tulikubaliana kuwa tunamuunga mkono Lissu. Hivyo ni jambo la kushangaza kumuona tena Membe akikanusha makubaliano hayo. ’’

“Msimamo wa ACT wazalendo ni kumuunga mkono Tundu Lissu.’’ Alisema Maalim Seif

‘’Mimi kama mwenyekiti wa Chama ninafahamu hivyo na kiukweli upande wa upinzani mgombea anayeonekana anaweza kumshinda Magufuli ni Lissu”.

Maalim aliongeza kusema kuwa uamuzi huo si wake binafsi au msimamo wa Zitto bali ni wa chama.

Aidha ACT Wazalendo haimkatazi Membe kufanya kampeni kama alivyosema.

‘’Msimamo wetu kama chama ni kumuunga mkono mgombea mwenye nguvu ambaye ni Lissu huyu Membe hatujui ana nia gani?”

Hata hivyo Maalim alisema uamuzi wao hauna tofauti na wanasiasa wengine wa upinzani ambao walisema wanamuunga mkono Magufuli, ila ameshangaa kipindi wanasiasa hao walipotangaza Tume ilikaa kimya.

https://www.instagram.com/p/CGkMavFB0Zm/

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents