AwardsBurudani

Maandalizi Kili Music Award 2011

Kili_jukwaani

Maandalizi ya tuzo za Kilimanjaro Music Award ndiyo yanafikia ukingoni ilikupisha tamasha zima la liweze kufanyika siku ya juma mosi Mach26 kwa mwaka huu 2011. Nafasi za kupiga kura zilishatolewa sehemu mbalimbali, ili kila mmoja apate nafasi ya kumpigia  msanii anayempenda, ilikufanikisha kuwania tuzo katika kinyanyiro husika.

 

Hakika huwa ni siku ya furaha  kwa  msanii, ambaye amechaguliwa kuwa mshindi   katika moja ya tuzo alizokuwa akiwania, na ndipo anapojua amekubalika kinamna gani kwa watu wake ambao wamefanikisha kwa yeye kupata tuzo hiyo.

Msanii anayepata  tuzo hujijengea histori ya mwaka huo, ingawa wapo wasanii kila mwaka wanachukua tuzo na kutokuwa jambo la ajabu kupata tuzo, lakini bado inamletea furaha kwa tuzo hiyo.

Tofauti na miaka ya nyuma kama tulivyozoea, mwaka huu wameamua kujali wasanii wa ndani  ambao watatumika katika kutoa buludani siku hiyo, tamasha badala ya wasanii toka nje. Ni jambo ambalo wasanii wamelipenda na wadau mbalimbali wameonekana kuliunga mkono, kwakuwa wao ndiyo wahusika wa tuzo basi hata katika kutoa buludani itabidi wahusike kuliko kutoa wasanii nje na kisha kutofikia ile buludani watu walioitarajia kutoka .

Kili_Bendi
Vifaa vya bendi vikiwa tayari kwaajiri ya kutoa buludani kutoka kwa msanii husika

Kili_Mixer

Kili_mitambo_ya_video

dj Akirekebisha vifaa, ilivisije vikawachachafya watu siku ya tamasha.

Kili_mpangilio_wa_viti

Mpangilio wa viti upo namna hii, karibu..

Kill_Steji

Hapa wakisogeza vifaa kwaajiri ya kutengenezea ngazi ya steji

Kili_taa

Zamu ya taa kupanda juu,

Kili_Cinenema

Hata wakirekebisha chombo maalum kwaajiri ya Sinema ya ‘Live’

Kili_wasanii_Barnaba

Wasanii wakiwa nje baada ya kupata somo kidogo la kuijua na kuisoma steji,

Kili_wapambe

Kama kawaida hata msibani wapambe hawakosi, nasi tulikuwepo hapo kukuletea taarifa hii, ila kwa zaidi picha za  na  video za matukio  yote tuungane kesho kwaajiri ya Tamasha lenyewe.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents