Videos
Dole ya Mabeste ft. Deddy ni video bora ya Bongo Flava tangu mwaka uanze? Itazame hapa
Hatimaye video iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ya wimbo wa Mabeste aliomshirikisha Deddy, Dole leo imeachiwa. Video hii imeongozwa na kutayarishwa na muongozaji mpya kwenye game nchini, Nisher kutoka Arusha. Video hiyo inadhihirisha ni kwa kiasi gani director huyo amekuja kuongeza ubunifu katika utengenezaji wa video za muziki nchini.
“Kuna watu wana-nigusa sana nikisoma message zao Dah!! hadi machozi yanani-dondoka nikiwaza mambo mengi nliyopitia nikiwa Arusha hadi kutoboza juu hivi, Namshukuru Mungu sana,” ameandika Nisher baada ya kupokea pongezi nyingi kutoka watu walioina video hiyo.
Bila wasiwasi, Dole ni miongoni mwa video kali zaidi za muziki zilizotoka tangu mwaka huu uanze. Itazame hapo chini.