Burudani

Madee adai katuni ya Wolper kwenye video yake ni ‘mashallah’

Msanii Madee amesema ameridhika jinsi umbile la Jacqueline Wolper lilivyoweka kwa mfumo wa katuni katika video yake mpya ‘Sikila’ aliyomshirikisha Tekno kutoka Nigeria.

“Yeah, kwa sababu ni katuni ni kama comedy tu, inachekesha kwani hata mimi kile ni kichwa changu wewe umeridhika nacho?,  ndiyo tunasea hiyo ni comedy hakuna ukweli wowote ni kujaribu kufanya kitu kingine ambacho hakijawahi kufanyika, then maisha yaendelee,” Madee ameiambia Bongo5.

Katika hatua nyingine Madee amefafanua cover photo ya ngoma hiyo ambapo anaonekana yeye akiwa amesema na Wolper lakini msichana aliyesimama na Tekno hajaweza kujulikana.

“Huyo alikuwa anatakiwa awe Lulu, sasa huyo hajapatiwa kakosewa ndio maana yeye (mchoraji) akasema tuachane naye na tusijaribu kumtaja kwa sababu hajampatia. Tekno ni rafiki yake sana na Lulu kwa hiyo alikuwa anajaribu kutengeneza hicho kitu,” amesema Madee.

By Peter Akaro

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents