Burudani
Madee agoma kutimiza ahadi yake ya kuchoma moto gari Arsenal ikifungwa na Chelsea
Madee amejikuta katika wakati mgumu kutekeleza kile alichoahidi baada ya timu yake ya Arsenal jana kupokea kichapo cha bao moja kw amtungi na Chelsea.
Muimbaji huyo ambaye ni shabiki wa Arsenal aliwaahidi mashabiki wake kuwa endapo timu hiyo itafunga, atachoma gari lake moto.
Hata hivyo baada ya Jumapili timu yake kupokea kichapo hicho alishindwa kutimiza alichoahidi. Kupitia Twitter aliandika:
Sina utajiri huo. .mpk kufikia hatua yakuchoma gari. .na hata km ningekua tajiri vp. .nisingefanya upumbavu huo…
— Madee (@Madeeseneda) January 25, 2016