Habari

Magufuli amsimamisha kazi Mkurugenzi wa jiji la Dar

Rais John Pombe Magufuli amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa jiji la Dar es Salaam, Dr Wilson Kabwe.

2

Ametangaza uamuzi huo wakati akimalizia kuhutubia kwenye uzinduzi wa daraja la Kigamboni leo.

Kabwe amesimamishwa kazi kwa tuhuma za kuingia kwenye mikataba iliyosababisha hasara ya zaidi ya shilingi bilioni 3.

Akiwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Kabwe amehusika kwa kuiongezea kampuni ya utozaji ushuru wa parking jijini pamoja na ongezeko la kiwango cha faini halali ya shilingi 20,000/=hadi 80,000/=kwa kila kosa la wrong parking.

Akiongea na wananchi kwenye uzinduzi huo, Magufuli amesema wananchi wamelia kwa muda mrefu kutokana na ufisadi wa baadhi ya viongozi na kwamba zamu imefika kwa mafisadi kulia pia.

“Kwahiyo leo ni zamu ya Kabwe naye akalie kule na vyombo vianze kuchunguza hali halisi, wakimclear mimi sina tatizo, akikutwa kuna tatizo hatua zifuate, ndio maana hapa kazi tu.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents