Habari

Mahakama ya uhalifu ya kivita ICC kuwekewa vikwazo na Marekani endapo itaendelea kuwashtaki raia wake

Mahakama ya uhalifu ya kivita ICC kuwekewa vikwazo na Marekani endapo itaendelea kuwashtaki raia wake

Marekani imetishia vikwazo dhidi ya mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC ikiwa itaendelea na mikakati yake ya kuwashtaki raia wa Marekani.Mahakama hiyo kwa sasa inatathmini kuwafungulia mashtaka wanajeshi wa Marekani kwa madai ya kuwatesa wafungwa nchini Afghanistan.

Mshauri wa masuala ya usalama ya kitaifa John Bolton alisema mahakama hiyo sio halali na kuapa kuwa Marekani itafanya kila iwezalo kuwalinda raia wake.

Baada ya tamko hilo kutoka marekani ikumbukwe kuwa wakati fulani mwaka uliopita nchi tatu za Afrika – Burundi, Gambia na Afrika Kusini ziliashiria nia yao ya kujitoa kutoka mahakama hiyo ya kimatafa ya uhalifu wa kivita ICC. Kulikuwa na hofu kuwa nchi zaidi zingefuata.

Mwezi Oktoba mwaka 2016, Burundi na Afrika Kusini waliandika kwa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa kuelezea uamuzi wao wa kuondoka kutoka ICC.

Wakati huo, nchi ya Gambia ambayo ni nchi ndogo ambayo sehemu yake kubw iko ndani ya Senegal magharibi mwa Afrika ilitangaza kuwa ingejitoa. Lakini hatua hiyo ilifutwa mara wakati serikali mpya iliingia madarakani.

Tangu wakati huo hatua hatua za nchi za Afrika kujitoa kutoka ICC huzijafua dafu, hata baada ta Muunganoa wa Afrika kutoa kauli ya pamoja na kujitoa kutoka mahaka hiyo.

“Kundi la watu wasio na maaana,” rais wa Uganda Yoweri Museveni wakati mmoja aliielezea ICC, huku rais wa Rwanda Paul Kagame akisema kuwa mahakama haikuwa kwa minajili ya haki bali siasa zinazotajwa kuwa haki ya kimataifa.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ambaye wakati mmoja alikabiliwa na kesi katika mahakama hiyo alisrma makahama hiyo ni chombo ya siasa za dunia lakina sio kuhusu haki ilizotakiwa kuteleleza.

Kurodhika na mahakama hiyo kumetokana na hisia kuwa ICC ilikuwa inawalenga waafrika na haieshimu siasa na uhuru wa nchi za Afrika. Keshi kumi kati ya tisa zilizo, kwenye mahakama hiyo zinahusu nchi za Afrika.

Mahakama hiyoi inachunguza na kuwaleta hukumuni wale wanaohusika kwenye uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu, ikiingilia kati wakati mahakama za nchi haziwezi kuwahukumu.

ICC ilibuniwa chini ya mkataba wa Roma wa mwaka 2002 na imeungwa mkono na nchi 123 ikiwemo Uingereza.

Baadhi ya nchi za Afrika zimataja kuondoka kutoka mahakam hiyo zikisema kuwa inazionea nchi za Afrika.

Chanzo BBC.

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents