Habari

Majirani wa Mhe. Lissu wazungumza, angalia mazingira ya eneo la tukio (+Video)

Majirani wa mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki na Mwanasheria mkuu wa CHADEMA, Mhe Tundu Lissu wamefunguka kwa mara ya kwanza baada ya Mwanasheria huyo kushambuliwa kwa risasi na wasiojulikana.

Mhe. Tundu Lissu

Majirani hao ambao wengi wao wanaonekana wenye nyuso za huzuni kufuatia tukio hilo la kinyama wameitaka serikali kuimarisha ulinzi nchini kote huku wakijiuliza kuwa kama kiongozi mkubwa anafanyiwa hivyo je, hao watu wa kawaida watafanyiwa nini?

Bongo5 imepata nafasi ya kuonana na Uongozi wa eneo la Area D katika Manispaa ya Dodoma Mjini, eneo ambalo tukio lilipotokea ambapo uongozi nao umelaani tukio hilo huku wakikiri kuwa wananchi wao bado wana hofu ya tukio hilo licha ya kuwa ulinzi umeimarishwa kwa sasa.

 

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents