Makala: Nisher kuna ugumu wa kurejea, ila game bado inakuhitaji (+video)
Mwaka 2012 akiwa kama director mchanga anayechipukia kwenye game, Nisher alilazimisha macho yetu kutazama runinga ili kushuhudia video mpya ya Joh Makini ‘Sijutii’ ambayo aliifanya yeye.
Maswali yakawa ni mengi juu ya ubora wa video ile, ila maswali mengi zaidi yalitaka kujua juu ya aliyetengeneza video huyo. Ndipo jina la Nisher lilipochomoza na watu kuelewa jamaa ni wa Arusha na kazi zake anazifanyika huko huko A Town.
kwa sasa Nisher ni miongoni mwa waongozaji wa video wenye ushawishi mkubwa nchini, ana historia yake katika muziki wa Bongo Fleva lakini kwa sasa yupo kimya. Hata hivyo bado mchango wake unahitaji katika game, kazi ni kwake kuhakikisha anarejea ingawa safari hiyo ina changamoto zake.
Bongo5 imekuandalia makala hii kwa mfumo wa video.
By Peter Akaro