Habari
Makamu wa Rais afika nyumbani kwa Mh. Lugola kufuatia kifo cha mkewe (+Picha)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 3, Januari, 2018 amehani msiba wa Kamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola ambaye ni Mke wa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. Kangi Lugola kilichotokea tarehe 1/1/2018 jijini Dar es salaam.