Michezo

Malinzi na wenzake ngoma bado nzito

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi na Katibu Mkuu wa shirikisho hilo Selestine Mwesigwa wamerejeshwa tena mahabusu hadi Julai 31 mwaka huu shtaka lao litakaposomwa tena.

Rais wa TFF, Jamal Emil Malinzi na Katibu Mkuu wa shirikisho hilo Selestine Mwesigwa

Uamuzi huo umetolewa katika Mahakama ya Kisutu Jijini Dar es Salaam, ambapo ndipo mashtaka hayo yalifunguliwa mara ya kwanza na kuendelea mpaka sasa.

Mnamo Juni 27 mwaka huu, Malinzi na Mwesigwa walishikwa na Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) kwa kutuhumiwa na matumizi mabaya ya madaraka waliyokuwa nayo katika uongozi wao na kupandishwa mahakamani kwa mara ya kwanza mnamo Juni 29 na kusomewa mashtaka 28 yakiwemo kughushi na kutakatisha fedha kupitia akaunti ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania.

By Hamza fumo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents