Mama yao Psquare alifariki baada ya upasuaji wa moyo


Sababu ya kifo cha Josephine Okoye,mama wa nyota wa muziki wa R & B nchini Nigeria wa kundi la Psquare, Peter na Paul imejulikana.
Maelezo ya msemaji wa Psquare yamesema mama yao alifariki saa chache baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo nchini India.
Mrs.Okoye alipelekwa nchini India kwaajili ya kufanyiwa operation baada ya kukaa katika hospitali ya St.Nicholas ya nchini Nigeria kwa muda, ambayo ni miongoni mwa hospitali ghali nchini humo.
Wakati huo huo, watu maarufu wamekuwa wakimimika kwenye nyumba ya kifahari ya P-Square iitwayo Square Ville, kuungana na ndugu na jamaa kwenye msiba huo.
Mastaa wengi wametumia mtandao wa Twitter kuwapa pole wasanii hao kwa kumpoteza mama yao.
Rita Dominic ‏@ritaUdominic
My heart goes out to the Okoye family today. RIP Mrs. J. Okoye God be with you!
D’banj kokomaster ‏@iamdbanj
My sincere condolences go out to Peter, Paul and the entire Okoye family. May the Lord be a comfort and strength to you at this sad time.
Pamoja na watoto wanne aliokuwa nao, Mrs Okoye ameacha mjukuu mmoja kutoka kwa Peter Okoye aliyezaa na Lola Omotayo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents