Burudani

Dj Khaled anamjua Diamond, Je! tutegemee kolabo

Ukiachana na mambo mengine bado mambo yanamuendea vyema mkali wa Bongo Flava Diamond Platnumz.

Hii ni baada ya rapper mkali na kutoka Marekani, Dj Khaled alipoamua kum-follow hit make huyo wa ‘Eneka’ kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram.

Dj Khaled amekuwa akishirikisha wasanii wa Marekani katika ngoma zake na albamu, kitendo cha msanii huyo kum-follow Diamond kinaashiria muziki wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla umekuwa na unatambulika duniani.

Siku chache nyuma rapper Rick Ross na Dj Clue walipost picha ya Diamond katika ukurasa zao za Instagram baada ya msanii huyo kupata dili la kuwa balozi wa kinywaji cha Belaire kutoka kampuni ya vinywaji vikali ya Luc Belaire ya nchini Ufaransa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents