Habari

Mamilioni ya watu walazimika kukaa tena majumbani kufuatia Corona

Mamilioni ya watu ulimwenguni kote wamelazimika tena kukaa majumbani na kuepukana na usafiri kufuatia masharti ya kuepusha kusambaa kwa virusi vya corona.

TFSCB's rapid support to help countries respond to the COVID-19 ...

India ni miongoni mwa nchi ambazo zimerudisha masharti ya kuzuia usafiri wa watu mnamo wakati maambukizi ya virusi vya corona yanazidi kuongezeka.

Tangu mwanzo wa mwezi Julai, takriban maambukizi mapya milioni 2.5 yamerekodiwa ulimwenguni kote, idadi hiyo ikiwa maradufu ya maambukizi yaliyotokea katika muda wa wiki sita kabla.

Hayo ni kulingana na ujumuishaji wa takwimu rasmi uliofanywa na shirika la habari la AFP. Nchini Marekani, jumla ya maambukizi 63,262 yamerekodiwa katika saa 24 zilizopita.

Kulingana na takwimu za Chuo Kikuu cha John Hopkins jumla ya watu 850 pia wamefariki nchini humo katika saa 24 zilizopita kutokana na COVID-19.

Takriban watu milioni 13 ulimwenguni kote wamethibitishwa kuambukizwa virusi hivyo na zaidi ya watu 570,000 wamefariki.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents