Michezo
Man United, Cazorla na baadhi ya nyota wa soka watuma salamu za pole kwa Danny Welbeck
Kiungo wa klabu ya Villarreal inayoshiriki La Liga, Santi Cazorla ametuma salamu za pole kwa Danny Welbeck baada ya kupata majeraha wakati akiitumikia Arsenal hapo jana kwenye mchezo wao wa Europa league dhidi ya Sporting Lisbon uliyomalizika kwa sare ya 0 – 0.
Cazorla ambaye amewahi kucheza timu moja na Danny Welbeck akiwa Arsenal amewaongoza baadhi ya nyota wengine kwenye mitandao ya kijamii kumtaka apone haraka majeraha hayo aliyopata.
Kwenye posti hiyo, Cazorla amesema ”Nakutaka uimarike haraka rafiki yangu, hili ni tukio baya zaidi katika soka lakini naamini upo imara na utarejea hivi punde.”
Wishing @DannyWelbeck a full recovery from his injury. #MUFC https://t.co/eONjpEEiSI
— Manchester United (@ManUtd) November 9, 2018