Michezo

Man United, City na Juventus vitani kumuania Harry Kane, wachezaji wengine wanao waniwa hawa hapa

Manchester City na Manchester United zitashindana katika kumuwania mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane, 26, kwa dau la paundi milioni 150 mwisho wa msimu huu (90min)

Juventus inataka kumsajili mshambuliaji wa England Kane mwisho wa msimu huu ili kucheza pamoja na Cristiano Ronaldo. (Tuttosport – in English)

Borussia Dortmund itamwachilia Jadon Sancho mwisho wa msimu huu iwapo atahitaji uhamisho. Winga huyo wa England 19 ananyatiwa na Liverpool , Man United na Chelsea. (Standard)Jadon Sancho

Mshambuliaji wa klabu ya Dortmund Jadon Sancho

Chelsea na Tottenham zote zinamnyatia kipa wa Bournemouth Aaron Ramsdale, 21. (Mail)

Klabu zote mbili pia zinamsaka Jeremie Boga, 23. Winga huyo wa Ivory Coast – mchezaji wa zamani wa Chelsea – atagharimu £13m kutoka klabu ya itali ya Sassuolo , huku Borussia Dortmund na Valencia pia zikivutiwa. (Sun)

Arsenal na Spurs zinatarajiwa kushindana katika kumsaini kiungo wa kati Marcel Sabitzer kutoka katika klabu ya RB Leipzig.

Mchezaji huyo wa Austria , mwenye umri wa miaka 25, alifunga magoli mawili dhidi ya Spurs katika ligi ya klabu bingwa siku ya Jumanne. (Calcio Mercato – in English)Marcel Sabitzer

Arsenal na Spurs zinatarajiwa kushindana katika kumsaini kiungo wa kati Marcel Sabitzer

Spurs pia inataka kumsajili mchezaji wa Real Madrid Eder Militao kwenda London kaskazini. Real kulipwa paundi milioni 70 ili kumuuza beki hiyo wa Brazil, 22. (El Desmarque – in English)

Pierre-Emerick Aubameyang anasema kwamba anafurahia kusalia Arsenal. Kumekuwa na uvumi unaomuhusisha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 na uhamisho wa kuelekea Barcelona. (Mirror)

Bayern Munich inamnyatia mchezaji wa Chelsea Willian. Kandarasi ya Kiungo huyo wa Brazil mwenye umri wa miaka 31 inakamilika mwisho wa msimu (Sun)Willian

Bayern Munich inamnyatia mchezaji wa Chelsea Willian.

Chelsea itajaribu kumsaini beki wa Brazil na Porto Alex Telles, 27, iwapo watefeli kumnunua mchezaji Ben Chlwell. Mchezaji huyo wa Leicester, mwenye umri wa miaka 23 ndio beki wa kushoto ambaye ni chaguo la msimu ujao. (Star)

Aston Villa na West Brom wote wanataka kumsaini mchezaji Karlan Grant kutoka Huddersfield. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 amefunga magoli 16 katika ligi hiyo msimu huu (Sky Sports)

Shirikisho la soka nchini Ufaransa linamtaka mshambuliaji wa PSG Kylian Mbappe, 21, kuichezea Ufaransa mwisho wa msimu katika michezo ya Olimpiki mjini Tokyo Japan.. (L’Equipe – in English)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents