Michezo
Man United, Liverpool, Man City hati hati kuvaana na Barcelona hatua ya 16 bora ya UEFA
Klabu za Liverpool, Man United na Man City vipo katika nafasi kubwa kupangiwa na Mabingwa wa Hispania FC Barcelona kwenye hatua ya 16 bora ya klabu bingwa barani Ulaya.
Katika hatua hiyo Barcelona haitakutana na klabu yoyote kutoka Hispania, wala na Spurs ambao wote walikuwa kundi B kwenye hatua ya makundi.
Klabu nyingine ambazo zinaweza kupangiwa na Barcelona ni AS Roma, Juventus, Ajax, Bayern Munich au Lyon.
Droo ya 16 bora itachezwa Jumatatu ijayo Desemba 17 mjini Nyon nchini Uswisi.