Michezo
Man United yamaliza vibaya ziara ya US kwa kichapo cha 2-0 toka kwa PSG
Manchester United wamemaliza ziara ya Marekani vibaya kwa kupokea kichapo kutoka kwa Paris Saint-Germain, PSG.
Wachezaji Zlatan Ibrahimovic na Blaise Matuidi walipeleka kilio hicho kwa Manchester United kwa kuifunga mabao 2-0.
Mchezo huo uliochezwa jijini Chicago ulikuwa wa mwisho na Manchester wanajiandaa na ufunguzi wa ligi kuu msimu 2015-16 Agosti 8, 2015. kwa kupambana na Tottenham.
Wachambuzi wa soka wamedai kuwa mlinda mlango David de Gea hakuwa katika ubora wake katika mechi hiyo.