Uncategorized
Manara afunguka kuhusu AS Vita ‘Ni kufa au kupona, lazima afe Taifa, wasanii wote wakubwa nitakuja nao’ (+video)
Msemaji wa klabu ya Simba Haji Manara amesema kuwa watahakikisha wanaibuka na ushindi kwenye mchezo wao wa mwisho wa hatua ya makundi wa michuano ya mabingwa barani Afrika dhidi ya AS Vita kutoka Congo. Huku afisa habari huyo machachari zaidi hapa nchini akisisitiza mashabiki na wapenda soka kujitokeza kwa wingi siku ya Jumamosi uwanja wa Taifa na kusema kwa msisitizo kuwa atahakikisha atakwenda na wasanii wote wa filamu na muziki kwenye mtanange huo utakao fanyika tarehe 16/03/2019.