Michezo
Manchester City imekamilisha usajili wa nyota wa Valencia, Nicolas Otamend
Klabu ya Manchester City hatimaye imekamilisha usajili wa mlinzi wa kimataifa wa Argentina, Nicolas Otamendi aliyekuwa mchezaji wa Valencia kwa dau la pauni milioni 32. Kocha mkuu wa klabu hiyo, Manuel Pellegrini anaamini kuwa amenunua beki bora zaidi.
Otamendi alifuzu vipimo vya afya na kukubali kusaini mkataba wa miaka mitano. Kabla ya hapo Otamendi alikuwa akihusishwa kutua Manchester United na Real Madrid.