Manchester City wachukua ubingwa wa Capital One
Klabu ya Manchester City wameshinda Kombe la Capital One baada ya kuwashinda Liverpool kwenye fainali kupitia mikwaju ya penalti baada ya dakika 120 kumalizika.
Katika mchezo huo uliokuwa mkali na wa kusisimua, Fernandinho alianza kuifungia Manchester City dakika ya 49, kabla ya Philippe Coutinho kuisawazishia Liverpool dakika ya 83.
Shujaa alikuwa ni kipa wa Man City, Willy Caballero aliyeokoa penalti tatu na kuipa taji la Capital One kikosi cha Manuel Pellegrini, baada ya kiungo Yaya Toure kufunga penalti ya mwisho.
Emre Can pekee alifunga penalti ya Liverpool, wakati za Lucas, Philippe Coutinho na Adam Lallana zilichezwa na Caballero, huku za City zikitiwa nyavuni na Sergio Aguero, Jesus Navas na Toure, baada ya Fernandinho kukosa ya kwanza.