Michezo

Manchester City yakutana na kisiki cha mpingo EPL, Guardiola aomba ‘VAR’ Premier League

Mabingwa watetezi wa ligi kuu England klabu ya Manchester City imejikuta ikihaha kutafuta sare baada ya kupigwa bao la mapema dhidi ya Wolves mchezo uliyomalizika kwa goli 1 – 1.

Kikosi cha Man City ambacho kinaaminika kuwa miongoni mwa timu bora zaidi msimu huu imejikuta ikipata bao la kusawazisha dakika ya 69 kupitia kwa mchezaji wake, Aymeric Laporte baada ya kufungwa bao la mapema kupitia kwa Willy Boly dakika ya 57 kipindi cha pili.

Boly gave Wolves the lead in controversial fashion, handling in from close range

Kwa matokeo hayo yanaifanya City ikipoteza alama mbili msimu huu huku Wolves ikifanikiwa kujikusanyia ponti mbili kwenye michezo yake mitatu iliyocheza.

Meneja wa Man City, Guardiola amesema kuwa licha ya kuonyesha mchezo mzuri ila anadhani kungepaswa sasa EPL kutumia mfumo wa VAR.

“Bila shaka Wolves wanastahili pongezi kuhusu goli lao siyo biashara yangu kulizungumzia hilo ila kwa namna yoyote ile Premier League  inapaswa kuanza kutumia mfumo wa VAR. Wakati nazungumza na mwamuzi nilikuwa naonekana kama kama kuingilia kazi yao ,” amesema Guardiola.

Kikosi cha klabu ya WolvesPatricio (8), Coady (6), Bennett (7), Boly (8), Doherty (6), Neves (6), Moutinho (7), Jonny (7), Jota (7), Jimenez (7), Costa (7).

Wachezaji wa akibaTraore (7), Vinagre (NA)

Kikosi cha klabu ya Man CityEderson (6), Walker (5), Kompany (7), Laporte (7), Mendy (6), Fernandinho (6), David Silva (6), Gundogan(7), Bernardo Silva (6), Aguero (6), Sterling (7).

Wachezaji wa akibaJesus (6), Sane (5), Mahrez (NA)

Mchezaji bora wa mchezo huo akiwaWilly Boly

 

Related Articles

One Comment

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents