BurudaniMichezoUncategorized

Manchester United kufanya mazungumzo na Leicester City kuhusu Harry Maguire

Klabu ya Uingereza  Manchester United imetumia ombi la kumsajili Harry Maguire mwenye umri wa miaka 25 kwa paundi milioni 65 kutoka Klabu ya Leicester City kwa mujibu wa mtandao wa Sky Sport.

Jose Mourinho ameonekana kuwa na shauku kubwa ya kunasa saini ya mchezaji huyo tegemezi wa Leicester City ikiwa ni siku chache kabla dirisha la usajili kufungwa.

Mashetani hao wekundu ametenga kitita cha paundi milioni 65 ili kunasa saini ya nchuzaji huyo ambaye alifanya kazi kubwa katika kikosi cha Uingereza ndani ya kombe la dunia.

Maguire anadaiwa bado yupo mpumzikoni na akirejea atatua moja kwa moja kwenda Old Trafford.

Hata hivyo,Leicester amepoteza Riyad Mahrez katika dirisha hili baada ya kumuuza mchezaji wa huo kwenda Man City.

By Clinton Abraham Sumari

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents