Manchester United kumtambulisha Sanchez ndani ya saa 24
Manchester United inatarajia kumtambulisha mshambuliaji wao mpya Alexis Sanchez ndani ya saa 24 zijazo baada ya kumaliza kupima vipimo vya afya hapo jana siku ya Jumapili huku tayari picha rasmi zimeanza kuonekana katika mitandao.
Mshambuliaji huyo raia wa mwenye umri wa miaka 29 anakuwa mchezaji anayelipwa fedha nyingi zaidi ndani ya klabu hiyo ambayo ni paundi 600,000 kwa wiki mshahara paundi 350,000, haki ya matangazo paundi 100,000 na paundi 144,000 kama nyongeza.
Alexis Sanchez akionekana akipiga picha ndani ya Manchester United
Usiku wa jumapili picha Sanchez ikimuonesha akipiga selfie ndani ya United akiwa amevaa jezi yake yenye jina ilianza kuenea katika mitandao mbalimbali.
Sanchez akiwa katika uwanja wa mazoezi wa Carrington ndani ya Manchester United kwaajili
Sanchez akiwa katika ndege binafsi akielekea Manchester siku ya Jumapili akitokea Kent Biggin Hill airport, kabla ya kutua United
Meneja wa United, Jose Mourinho siku ya Jumamosi amesema kuwa kilakitu kimekwenda sawa kinachosubiriwa ni kutambulishwa ndani ya saa 24.
Sanchez ameposti Video zikimuonesha akiwa katika ndege binafsi akielekea Manchester
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amesema, kuondoka kwa Sanchez kipindi hiki cha mwezi Januari imekuwa swala gumu sana kwa upande wetu, hii ni kwamara ya kwanza inatutokea upande wetu mwezi huu wa kwanza. “Tunawachezaji wakubwa ambao wazuri hivyo sikumuhusisha Sanchez dhidi ya Palace kwakuwa yupo mbioni kwenda United,”amesema Wenger.
Henrikh Mkhitaryan akisherehekea siku yake ya kuzaliwa akiwa na wakala wake Mino Raiola na mchezaji mwenzake Paul Pogba huku akiposti picha yake kupitia mtandao wa Instagram