Michezo
Manchester United waipa shavu Tanzania kwenye Instagram
Hii ni habari njema kwa mashabiki wa Manchester United nchini baada ya club hiyo kupost picha ya mchezaji wa zamani wa timu hiyo Andy Cole akiwa na watoto wa Tanzania.
Mchezaji wa zamani wa Manchester United Andy Cole akiwa Tanzania hivi karibuni katika mchakato wa kulichangia shirikisho la mpira wa miguu Tanzania pia kuitangaza Tanzania.
Manchester wameandika:
MUFC ambassador and goalscoring legend Andy Cole has been in Dar es Salaam in Tanzania, helping with a project to donate footballs to the Tanzania Football Federation. Good work Andy!”.
Cole alikuwa nchini kwa siku mbili kusaidia maendeleo ya soka na kushiriki kwenye kampeni ya ‘Mimi ni Bingwa’ iliyofanyika Coco Beach jijini Dar.